Wadau wa Utalii wakiwa katika Viwanja vya Nane Nane
Wa Kwanza Kulia mkuu wa Wilaya Mbeya Rashidi Chuachua akipokea Maandamano ya wadau wa utalii katika eneo la Mnara wa Mashujaa
Wadau wa Utalii wakiwa Kisiba Campsite
Maporomoko ya Maji Kapologwe
Ndani ya Ukumbi wa Mkapa
Wiki ya Utalii Mkoani Mbeya iliadhimishwa kwa kuwa na mfululizo wa matukio mbalimbali kama ifuatavyo
Tarehe 21/09/2021
Ziara katika vyombo vya habari ikiwemo Redio, Televisheni ilimkuhamasisha na kutoa elimu kwa wananchi juu ya umuhimu wa utalii
Ziara katika vyombo vya habari ikiwemo Redio, Televisheni ilimkuhamasisha na kutoa elimu kwa wananchi juu ya umuhimu wa utalii
Tarehe 22/09/2021
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma zuberi Homera alifanya press ya ufunguzi wa wiki ya Utalii Mkoani Mbeya.
Tarehe 24/09/2021, Siku ya Ijumaa
Wadau wa utalii walifanya Road show kuanzia nane nane Mbeya mpaka Mnara wa mashujaa ambapo msafara huu ulipokelewa na mkuu wa Wilaya Mbeya Rashidi ChuaChua
Tarehe 25/09/2021, Siku ya Jumamosi
Wadau kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa walifanya Safari ya kitalii kwenda KISIBA CAMPSITE, kabla ya kufika walitembelea Mti Mkubwa wa Katembo uliopo masoko ambao ili kuuzunguka unahitaji kwatu 12 wakiwa wameshikana mikono, na kisha baadae kuelekea Kisiba Campsite wapo wadau walirudi Mbeya lakini wapo wadau walifanya Camping
Tarehe 26/09/2021, Siku ya Jumapili
Asubuhi wadau waliamka na kufanya michezo mbalimbali na kisha kuelekea Maporomoko ya maji Kapologwe kisha kuelekea Mbeya.
Tarehe 27/09/2021, Siku ya Jumatatu
Tulikutana katika ukumbi wa mkapa kwa ajili ya kufanya Tathimini ya wiki ya utalii
Shughuli hii ilipewa nguvu na UPL SAFARIS, EVERDAY MBEYA, KISIBA CAMPSITE, UTALII NA KALAMU,
UTENGULE COFFEE LODGE, PHOENIX HOTEL, G TOWN HOTEL, HILL VIEW HOTEL, BUSOKELO
TV NA BONGE GARAGE
Comments
Post a Comment