UZINDUZI WA SIKU YA UTALII NA KALAMU MKOANI MBEYA

Wa kwanza kushoto Muwakilishi kutoka ofisi ya RPC mkoa wa Mbeya, Wa pili Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Ileje Haji Mnasi na anayefuata Ni Mgeni rasmi Katibu Tawala Mkoa Wa Mbeya Dr. Anjelina Lutambi.

Fadhy Mtanga Msafiri na Mwandishi wa Riwaya Mbalimbali baadhi ya Riwaya hizo ni pamoja na Huba, Fungate, na Rafu, Akiwa kama mmoja wa watoa na maada alianza kwa Kumpongeza Bi Macrina Ntabagi kwa uzinduzi huu wa jarida la utalii pamoja na kueleza umuhimu wa kutangaza utalii Mkoani Mbeya

Hon Ipyana Mwakyusa akizungumza na wadau wa utalii ukanda wa Nyanda za juu kusini, alijikita zaidi katika kueleza namna ambavyo vijana wanaweza kuchangamkia fursa zikizopo katika sekta ya utalii pia aliongeza kwamba vijana waweze kuitumia teknolojia ili kujitengenezea kipato wao na kukuza uchumi wa Nchi kwa Ujumla.

Richard Musingi Salagata Afisa Biashara Mkoa Wa Mbeya, alimpongeza Bi Macrine Ntabagi kwa wazo la kibunifu, ambapo alieleza umuhimu wa wadau kurasimisha biashara zao, umoja lakini pia kulitumia Jarida Hili kwa ajili ya kutangaza shughuri zao.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje Haji Mnasi akitoa salamu za pongezi na kueleza vivutio vya kitalii pamoja na fursa za uwekezaji zipatikanazo katika Halmashauri ya Wilaya ya Ileje.

Gabriel Shawa Mkurugenzi wa UPL Safaris akitoa salamu kwa niaba ya wadau na watoa Huduma za utalii katika mkoa wa Mbeya.
 
Amos Asajile Mratibu wa Uyole Cultural tourism Enterprise pamoja na Mkurugenzi wa Kisiba Campsite aliyekuwa mmoja wa watoa maada akielezea Historia ya Mkoa wa Mbeya na Hali ya utalii katika Mkoa wa Mbeya.
Mgeni Rasmi Dr Anjelina Mageni Lutambi Katibu Tawala wa Mkoa wa mbeya aliye muwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Comrade Juma Zuberi Homera.

Mgeni Rasmi Akizindua Rasmi jarida la M Magazine 



Baadhi ya wadau wa utalii Katika Mkoa wa Mbeya wakiwe kwenye picha ya pamoja na Mheshimiwa Mgeni Rasmi pamoja na meza kuu


Baadhi ya wadau wakiwa katika picha moja na Mgeni Rsmi pamoja na Meza kuu.

Uongozi wa Jarida la Mbeya Advertise with Macrine mnamo tarehe 26/06.2021 ulizinda Jarida la utalii katika ukumbi wa Usungilo Hotel Uliopo Mbeya Mjini.

Siku ya utalii na Kalamu uliambatana na uzinduzi wa Kampeni ya utalii itakayogusa vijana wa shule wenye ari chanya katika ukuaji wa utalii, Pamoja na Jarida la kutangaza Fursa mbalimbali nchini Tanzania.

Hafla hii ya uzinduzi ilihudhuliwa na wadau mbalimbali wa utalii katika ukanda wa Nyanda za Juu kusini mwa Tanzania, Baadhi ya wadau hao ni Bodi ya Utalii ofisi ya kanda iringa, Mamlaka ya wanyama pori Tanzania TAWA, Hifadhi ya Taifa Kitulo, pamoja na wadau mbalimbali kutoka ndani na nje ya mkoa wa Mbeya.

mnamo juni mwaka 2018 tulifanikiwa kuzindua jarida letu la utalii lililokuwa limejikita zaidi kuibua fursa na kutangaza utalii wa Nyanda za juu Kusini mwa Tanzania, baada ya kufanya utafiti na kutambua fursa mbalimbali zilizopo katika nchi yetu, uongozi wa jarida umeamua kupanua wigo wa matangazo katika fursa mbalimbali za utalii, uwekezaji na biashara Kutoka nyanda za juu Kusini na kuwa Tanzania Nzima. Kwa sasa jarida hili litajulikana kama M MAGAZINE, Jarida hili linategema kusambazwa kama FREE MAGAZINE kwenye ofisi mbalimbali za uma na taasisi binafsi "alieleza Bi Macrine Ntabagi"

Akaongeza kwa kusema Pamoja na mafanikio makubwa katika kuwafikia watanzania wengi, uongozi umeamua kuwa na kampeni rasmi inayoitwa UTALII NA KALAMU, tukiwa na maana utalii unaongezwa ubunifu na kuenzi maandishi, katika kampeni hii tutakuwa na mijadala mbalimbali, CLUB za utalii, na mashindano kwa wanafunzi ili kupata wanafunzi wwenye uelewa katika masuala ya utalii watakao kuwa mabalozi wazuri wa utalii kwa siku za mbeleni.

Dr Anjelina Lutambi akijibu lisala iliyosomwa na Mkurugenzi wa Utalii Bi Macrine, alisisitiza ushirikiano baina ya wadau, kutafuta eneo ambalo itaweza kuwekwa information centre itakayoweza kurahisisha upatikanaji wa taarifa za utalii, lakini pia kutoa ushirikiano kwa wadau wote wa utalii, kukaa pampoja na wadau pamoja na kurudisha kamati za utalii za wilaya na Mkoa, akizungumza kuhusu miundombinu alisema Ofisi imejipanga na kuahidi kwamba suala la Miundombinu si muda mrefu itabaki historia.

 

Comments