Maporomoko ya Maji Kimani/ Kimani waterfalls

Muonekano wa Maporomoko ya Maji Kimani


Godwin Mwambaja muungoza watalii (Tour Guide) Kutoka Uyole Cultural Tourism Enterprise Akipunga upepo Mara baada ya kuogelea katika pool ya Maporomoko ya Maji ya Kimani

Siku ya Ijumaa Tarehe 05/06/2021 Tulifanya safari ya kutembelea pori la akiba la Mpanga Kipengere na kupiga kambi tukitokea Mkoani Mbeya. katika safari hii tuliambatana na Mazplusfly, Photo Bank studios Pamoja na Busokelo Tv

Pori la Akiba la Mpanga/Kipengele linapatikana nyanda za Juu Kusini mwa Tanzania katika Mkoani Mbeya Wilaya ya Mbarali, na Mkoa wa Njombe Wilaya ya Wanging’ombe na Makete. Pori Lina ukubwa wa Kilomita za Mraba 1574 kwenye mwinuko wa mita 1300 – 3000 kutoka usawa wa Bahari. Pori hili linasimamiwa na Mamlaka ya usimamizi wanyama Pori Tanzania (TAWA)

Maporomoko ya Maji Kimani yanapatikana ndani ya Pori la Akiba la Mpanga/Kipengere umbali wa Kilomita kumi na tatu (13) Kutoka Barabara Kuu ya Mbeya – Iringa, muonekano wa maporomoko haya unavutia sana kutokana na namna maji haya yanavyo anguka katika mwamba wenye ngazi ngazi pamoja na uwepo wa sehemu za kuogelea. Unaweza kufanya utalii wa kupanda miamba (Rock climbing), Kuogelea (Swimming), kupiga picha (Video & Photo Graphing) N.K

Vivutio vingine Vipatikanavyo katika Pori la Akiba la Mpanga Kipengere ni Pamoja na

1.  Maporomoko ya Maji saba (7) ambayo ni Kimani, Nyaugenge, Lyamakonokwila, ikovo, Kipengere, merere, na Allan

2. Pango La Chifu Mkwawa, lililopo Karibu kabisa na maporomoko ya maji ya Kimani, Ambalo lilitumika kama sehemu ya maficho ya Chifu Mkwavinyika Munyigumba Mwamuyinga (Mkwawa) kiongozi wa kabila la Wahehe.

3. Bafu la Chifu Mkwawa, lililopo katika Mto Kimani mita chache Kutoka lilipo pango la Chifu Mkwawa, Bafu lina ngazi mbili alizokuwa akizitumia kushuka na kupanda.

4. Kisugulio, Jiwe alilolitumia chifu Mkwawa

5. Mabaki ya Mafiga, Yapo Mawe Matatu yanayofanya Mafiga yaliyotumika kuchoma na kupikia vyakula.

6. Jiwe la Kusagia, jiwe hili lilitumika na chifu mkwawa kusagia nafaka ikiwemo Uwele, Mtama, Chumvi/Magadi, Vyakula na dawa za Mizizi.

7. Fuvu La Nyani, aina ya Yellow Baboon Lililohifadhiwa ndani ya pango la Chifu Mkwawa.

8. Zana za Kale zilizotumika na Chifu Mkwawa.

9. Mkusanyiko wa Mawe ya Kubisha hodi

10.Uoto wa Asili. Wenye miti aina ya Miombo

11.Kipembo, neno la kiwanji lenye maana ya “Jivu” ni eneo la Njia ya watumwa lililotumika kuwachoma moto watumwa waliokuwa wamechoka na wagonjwa.

12.Aina mbalimbali za miamba

13.Ukanda wa Maua ya Asili aina ya (Orchid) katika eneo la Ibaga

  Shukrani za dhati kwa uongozi wa TAWA kwa mapokezi, Huduma na ushirikiano mkubwa tulioupata Ambrosy Mng’ongo  Kamishna msaidizi mwandamizi TAWA, Joas Makwati Meneja Mpanga Kipengere na Leonard Nsajigwa Askari Muongoza Watalii 

Photo Credit & Drone Operations: Mazplusfly

Photo Credit & Video:Photo Bank Studios 

Makala & Guiding: Chikanda safaris & Adventure

MediaBusokelo Tv (Subscribe Busokelo Tv, ili usipitwe na habari moto moto za utalii na utamaduni pamoja na habari Zinginezo)


Karibu Mbeya | Karibu Tanzania

Help us to share with your friends, For more tourism updates follow us on the following social networks

Things to do in Mbeya | Mbeya tourist atractions | Chikanda safaris & Adventure

Comments